![]() |
Washauri wa maendeleo binafsi (Self Development) wanatuambia kwamba mikakati (strategies) huchangia asilimia 20 tu ya mafanikio ya mtu. Asilimia
80 hutokana na maandalizi ya kisaikolojia.
Hii ina maana
kwamba maandalizi bora ya kisaikolojia ndiyo huchukua nafasi kubwa katika
kufanikisha malengo yako.
Lakini wengi
wetu tunakwenda kinyume. Tunapanga mikakati 100% na kusahau kabisa suala la
saikolojia na wengine hatuna kabisa habari na kitu hiki.
Tunafikiri kwamba
tukiwa na mikakati mizuri tu tutafanikiwa.
Mikakati
inaposhindwa kukufikisha kwenye malengo, unaanza lawama; “sina bahati… nimehujumiwa…serikali yetu haina sapoti…” tunalaumu
ndugu na jamaa, tunalaumu wafanyakazi wenzetu, tunalaumu ndugu na jamaa na
marafiki.
Hatutaki
kuwajibika na matokeo yetu. Badala ya kukubali mapungufu yetu, kuzipokea
changamoto na kuzifanyia kazi,
tunatafuta mchawi wa kumbebesha mzigo wa lawama.
Na kisha
tunajiridisha kwa kuwachukulia wale waliofanikiwa kuwa hawakutumia njia halali.
Wamehonga, wametoa rushwa, washirikina, mafreemason nk.
Kuanguka au
kufanikiwa kwa mtu huanzia kwenye fikra zake.
Haijalishi askari ana mbinu kali au silaha bora kiasi gani, akiingia
vitani na fikra za kushindwa, atashindwa tu.
Fikra ndio
kila kitu. Weka fikra chanya kwenye malengo yako utaona mikakati inafanya kazi.
Weka fikra hasi, utaona mikakati inakwama.
Mikakati ni
nyenzo tu za kukuwezesha kuyafikia malengo yako. Nyezo pekee yake haziwezi
kukufikisha unakotaka kwenda kama haukotayari au hujajiandaa kisaikolojia.
Fikiria kuwa unataka kwenda ghorofa ya kumi na ngazi ndiyo nyenzo pekee ya kukufikisha,
bila kujiandaa kisaikolojia utapataje msukumo na nguvu ya kupanda hizo ngazi?
Kuna
maandalizi mengi ya kisaikolojia, hapa nitagusia baadhi tu.
Uchu/shauku. Moyo wako ukitawaliwa na
shauku kali ya kufanikisha malengo yako utakuwa na nguvu na msukumo wa kimwili
na kiakili wa kuitumia mikakati yako
kukufikisha kwenye malengo yako.
Bila kuwa na uchu/shauku kubwa ni rahisi kukata tamaa na kuvunjika moyo
endapo utakutana na vikwazo hata kama ni vidgo tu. Hutakuwa na moyo wa
kupambana.
Kujiamini. Jiamini wewe mwenyewe kuwa
unaweza na kile unachokitaka kuwa kinawezekana. Unapojiamini unakuwa na nguvu
na unajiweka karibu na malengo yako.
Unapokuwa na hofu unakuwa dhaifu
na unajiweka mbali na malengo yako. Kujiamini ni kuwa na mtazamo chanya wa
kufanikiwa kwa kile unachokifanya.
Imani. Ondoa imani zote potofu juu ya kile
unachokitaka. Unapokuwa na imani zinazokinzana baina ya fikra na malengo, si rahisi kufanikiwa. Kwa mfano, watu wengi tuna imani potofu kuhusu pesa
ilihali tunazitaka kwa hali na mali. Methali hizi kuhusu pesa zinakinzana; pesa asali ya roho/pesa chanzo cha matatizo.
Watu wengi tunaamini kuwa pesa hupatikana kwa kazi ngumu. Imani hujenga. Ukiamini kuwa pesa ni ngumu basi itaendelea kuwa ngumu. Ukiamini
kuwa pesa ni rahisi itakuwa rahisi tu. Ni imani tu. Ukiamini unaweza, utaweza.
Ukiamini huwezi hutoweza kamwe.
Kwa ujumla,
bila kuwa na maandalizi mazuri ya kisaikolojia, mikakati pekee haitasaidia
kukufikisha unakotaka. Ni muhimu kuwa na mikakati mizuri na maandalizi mazuri
ya kisaikolojia tunapopanga kufanikisha malengo yetu.
Mungu
akubariki.
.jpg)
0 comments:
Chapisha Maoni