Jumanne, 16 Desemba 2014

NGUVU YA MALENGO

Katika Kufikia Mafanikio.

Katika kitabu  cha “The Great Escape”,  mwandishi Geoff Thompson anazungumzia kitu kimoja kilichonigusa na  kuamua kukileta kwako, huenda kwa namna moja au nyingine kikakugusa pia. Kifupi anazungumzia nguvu ya malengo katika kufikia mafanikio.

Geoff , anazungumzia survey maarufu iliyofanyika miaka mingi ya nyuma katika chuo kikuu cha Harvard, miongoni mwa vyuo bora zaidi duniani. Survey ilihusu mambo mbalimbali ambayo mwanafunzi alitakiwa kuyatolea maoni yake. Matokeo ya survey hiyo yalisababisha mshituko mkubwa miongoni mwa wahadhiri wa Harvard hususani katika vipengere vifuatavyo;

  1.                Una malengo?
  2.         Una utaratibu wa kuandika malengo yako? 

Karatasi zilipokusanywa na majibu kupitiwa, wahadhiri walishangazwa. Wastani wa 15% ya wanafunzi ndio waliojibu kuwa wana malengo yoyote, na kati  kati yao pia ni wachache tu ndio waliojaribu kuandika malengo yao.

Hii ina maanisha kuwa zaidi ya asilimia 85 ya wanafunzi wote waliofanyiwa survey, walikuwa wanasoma bila malengo yoyote. (Ikumbukwe kuwa Harvard hujivunia kudahili wanafunzi bora zaidi nchini Marekani).

Pamoja na kwamba survey hiyo iliwashangaza na kuwakatisha tamaa wahadhiri wa Harvad, matokeo yalihifadhiwa.

Miaka mingi baadaye, katika mkutano wa wafanyakazi wa chuo hicho, mhadhiri mmoja aliibua wazo la kurudiwa kwa survey kama hiyo ili kuona kama kuna tofauti ya wanafunzi waliokuwa wanadahiliwa muda huo na kipindi cha nyuma.

Kabla hawajakubaliana kuchukua survey nyingine ulifanyika uamuzi wa kukusanya pesa kwa ajili ya kuwafuatilia waliofanyiwa survey ya kwanza kama kuna walichofanikisha maishani.
Wanafunzi waliofanyiwa survey ya awali walitafutwa. Wale walioandika malengo yao waliulizwa;

Umefanikisha malengo uliyojiwekea kipindi ukiwa mwanafunzi?

Na wale ambao hawakuandika malengo yao waliulizwa;
Maisha yako yanaendaje?

Cha kushangaza, waligundua kuwa asilimia 95 ya wale ambao hawakuandika malengo yao hawakufanikiwa chochote na hawakuwa wamefikia uhuru wa kifedha kama ilivyokuwa inatarajiwa kwa mtu aliyehitimu chuo kikuu (hasa Harvard).

Asilimia 80 ya wale waliojiwekea malengo walikuwa wameyafanikisha na kwa wale wachache ambao waliandika malengo yao walikuwa wamekwisha fanikiwa kufikia uhuru wa kifedha.

Hapa tunajifunza kuwa kujiwekea malengo ni utaratibu muri wa kufanikiwa maishani.

Watu wengi tunapuuza kujiwekea malengo kwa kufikiri kuwa majina makubwa ya vyuo tunavyosoma yatatufanya tufanikiwe. Pengine kwa kudhani kwa kuwa tunafaulu mitihani yote tunayofanya, tutafanikiwa bila malengo kuwa na yoyote.

Au tunafikiri kuwa tutafanikiwa kwa kuwa tunatoka katika koo na familia maarufu.

Kwa vyovyote vile kujiwekea malengo ni muhimu kama unataka kufanikiwa.

Mtu asiye na malengo ni sawa na meli au ndege inayoanza safari bila kujua inakoelekea. Utawezaje kufika mahali ambapo hujui palipo? Huwezi kufika kama hujui unakokwenda.

 Unaweza ukaanzisha safari ndefu, ukavumilia dhoruba kali kwa kuwa unafahamu unakokwenda, unapaona unakoelekea. Hata kama mambo yatakuwa magumu vipi, utaangalia mbele na kusema, “ninaona mwnga mbele, nimekaribia kufika.”

Hebu fikiria unapigwa na dhoruba kali katika safari ambayo hujui unakoelekea, kishawishi cha  haraka kitakuwa ni kurudi ulikotoka au kuelekea sehemu nyingine. 

Bila malengo mbele utaona giza na maluweluwe tu. Watu wengi tunakata tamaa na kushindwa kufikia mafanikio kwa sababu hatuna malengo.


Unahitaji Malengo.

0 comments:

Chapisha Maoni