MAFANIKIO NI KUTIMIZA NDOTO.
Swali la
kujiuliza ni kwamba, je, unaitambua ndoto yako?unaifanyia kazi ndoto yako? Kama hujafanya juhudi yoyote ya kuitambua na kuifanyia kazi ndoto
yako, watu wengine watakutumia ili kutimiza ndoto zao.
Kwa
kila tunachofanya, aidha tunafanya kwa
ajili ya kutimiza malengo yetu ama tunawatumikia wengine kutimiza malengo yao.
Ndoto yako
ndiyo itakayobainisha malengo yako maishani.
Ndoto ni wazo
lolote lililo kichwani mwako ambalo bado halijajidhihirisha katika ulimwengu
halisi.
Kichwani kwako unaweza ukawa na kitabu kizuri
ambacho bado hakijaandikwa, wimbo mzuri ambao bado haujaimbwa, daktari au
mwanasheria mzuri ambaye bado hajahitimu, biashara ambayo haijaanzishwa, ugunduzi
ambao haujawekwa hadharani, mchezaji mzuri ambaye bado hajaonekana na vitu
vingine kama hivyo. Hizi zote ni ndoto zinazotafuta nafasi katika ulimwengu
halisia.
Unapoingundua
ndoto yako na kuifanya kuwa lengo lako maishani, maisha huwa marahisi na yenye
furaha. Kazi inakuwa ni sehemu ya maisha badala ya kitu unachofanya ili uishi. Kila
kitu unachofanya kinakuwa ni kitu cha kukupatia furaha na kukamilisha malengo
yako.
Siyo kwamba
unapofuata ndoto yako ndiyo kila kitu kitakuwa rahisi, hapana. Utakutana na mambo
mengi tu ya kukuvunja moyo na kukatisha tamaa. Unachotakiwa ni kujipa moyo na
kusonga mbele.
Ndoto yako
inaweza kuchukua muda mrefu au mfupi kutimia kulingana na hatua unazochukua na
jinsi unavyozishughulikia changamoto zinazojitokeza.
Unaweza
ukawa na visingizio vingi na sababu za kutosha kuelezea kwa nini maisha yako
hayawi kama unavyotaka , lakini hutoweza kuwa na furaha wala kufikia mafanikio
ya kweli kama hutaitambua na kuifuata ndoto yako kuu.
Wewe ndiye mwenye
usukani wa maisha yako. Unataka kuwa nani, unataka uishi vipi, ufanye nini, ufanikishe
kipi, ni maamuzi yako mwenyewe na si ya
mtu mwingine.
Neno la Tahadhari:
Unapoamua kuchukua uamuzi wa kuifuata ndoto yako na kutimiza malengo yako, watu wengi watakukatisha tama, watakuvuta chini, watainanga ndoto yako na kuyapuuza mawazo yako.
Watasema kuwa uachokifikiria hakifai na kakiwezekani.
Watadai kuwa huna uwezo
wa kufanya unachotaka kufanya.
Unapowaambia wengine kuhusu malengo yako na vitu unavyotaka
kuvifanikisha maishani wengi watakukatisha tamaa. Wanachofikiri au kusema
hakijalishi. kila mtu aliyefanikiwa unayemfahamu wewe ana stori nyingi za
kukatishwa tamaa alizo kutana nazo pindi anafanya jitihada za kutimiza ndoto
yake.
Utakapoitambua
ndoto yako na kuamua kuifuata utafungua uwezo mkubwa uliomo ndani yako ambao
kukupata kuuona kabla. Utashangaa nguvu kubwa ikikusukuma na kukuongoza.
Unaifahamu
ndoto yako? unayajua malengo yako maishani?
Jaribu kuyatafakari maswali haya,
yape utulivu wa kutosha na tafakari ya kina. Jibu unaweza kulipata papo hapo
au likachukua muda, labda siku mbili, wiki, mwezi au mwezi kulingana na uzito
utakayoyapa.
Jibu maswali
haya;
- Kusingekuwa na kushindwa katika maisha, yaani tungekuwa tunafanikiwa tu kwa kila tunachokifanya, ungechagua kufanya nini au kuwa nani katika maisha yako?
- Ungepewa uwezo wa kimiujiza kubadilisha kitu kimoja hapa duniani papo kwa papo, kingekuwa ni kitu gani? Ungebadilisha nini?
- Fikiria kuwa umefanikiwa kifedha na huna haja ya kufanya kazi tena, huna haja ya kuwaza tena kuhusu pesa na una muda mwingi wa kufanya unachotaka. Je, ungetumia siku zako kufanya nini?
Kila la heri katika safari ya kutimiza ndoto zako!
.jpg)
0 comments:
Chapisha Maoni